Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 5:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate shida, Kama cheche za moto zirukavyo juu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Bali binadamu huzaliwa apate taabu, kama cheche za moto zirukavyo juu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Bali binadamu huzaliwa apate taabu, kama cheche za moto zirukavyo juu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Bali binadamu huzaliwa apate taabu, kama cheche za moto zirukavyo juu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zinavyoruka kuelekea juu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate shida, Kama cheche za moto zirukavyo juu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 5:7
11 Marejeleo ya Msalaba  

Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.


Je! Mtu hana huduma ngumu juu ya nchi? Na siku zake, je! Si kama siku za mwajiriwa?


Miaka ya maisha yetu ni sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Tena kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana wakati unapita upesi nasi kutokomea punde.


Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.


Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua?


Kwa kuwa siku zake zote ni masikitiko, na kazi yake ni huzuni; naam, hata usiku moyoni mwake hamna raha. Hayo nayo ni ubatili.


Nilitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?


Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili muweze kustahimili.