Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 5:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Heri mtu yule ambaye Mungu anamrudi! Hivyo usidharau Mungu Mwenye Nguvu anapokuadhibu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Heri mtu yule ambaye Mungu anamrudi! Hivyo usidharau Mungu Mwenye Nguvu anapokuadhibu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Heri mtu yule ambaye Mungu anamrudi! Hivyo usidharau Mungu Mwenye Nguvu anapokuadhibu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Heri mtu yule ambaye Mungu humkanya; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 5:17
14 Marejeleo ya Msalaba  

Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu, Na kumnyoshea mikono yako;


Je! Utulivu wa Mungu ni mdogo sana kwako, Maliwazo ya Mungu ni madogo sana kwako?


Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake, Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu.


Naam, yeye angekuongoza utoke katika msiba Hata mahali penye nafasi, ambapo hapana kizuizi; Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.


Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;


BWANA ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.


Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;


Hakika nimemsikia Efraimu, akijililia hivi, Umeniadhibu, nami nikaadhibika, kama ndama asiyeizoea nira; unigeuze, nami nitageuka; kwa maana wewe u BWANA, Mungu wangu.


Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo.


Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji la uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.


Angalieni, twawaita heri wao waliostahimili. Mmesikia habari za kustahimili kwake Ayubu, kuona mwisho Bwana aliyomtendea, jinsi Bwana alivyo mwingi wa rehema na mwenye huruma.


Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.