Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 5:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Yeye huitangua mipango ya wadanganyifu, Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huvunja mipango ya wenye hila, matendo yao yasipate mafanikio.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huvunja mipango ya wenye hila, matendo yao yasipate mafanikio.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huvunja mipango ya wenye hila, matendo yao yasipate mafanikio.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye huitangua mipango ya wadanganyifu, Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 5:12
23 Marejeleo ya Msalaba  

Hata siku ya tatu Labani akaambiwa ya kwamba Yakobo amekimbia,


Lakini Uria akalala mlangoni pa nyumba ya mfalme, pamoja na watumishi wote wa bwana wake, wala hakushuka nyumbani kwake.


Naye Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, Ushauri wa Hushai, Mwarki, ni mwema kuliko ushauri wa Ahithofeli. Kwa maana BWANA alikuwa amekusudia kuuvunja ushauri mwema wa Ahithofeli, ili BWANA alete mabaya juu ya Absalomu.


Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli, kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami.


Kisha ikawa, adui zetu waliposikia ya kuwa tumekwisha kupata habari, na ya kuwa Mungu amelibatilisha shauri lao, ndipo sisi sote tukarudi ukutani, kila mtu kwa kazi yake.


Bali sisi tulimwomba dua Mungu wetu, tena tukaweka walinzi, mchana na usiku, kwa sababu yao, ili kuwapinga.


Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako, Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.


Wakipanga kukutenda mabaya, Kwa miango ya hila, hawatafanikiwa.


Maana mikono ya wasio haki itavunjika, Bali BWANA huwategemeza wenye haki.


Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya BWANA.


Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa; Bali huyapindua maneno ya mtu haini.


Na roho yao Misri itaondolewa, nami nitaiharibu mipango yao, nao watakwenda kwa sanamu zao, na kwa waganga, na kwa wapiga ramli na kwa wachawi.


Basi malaika wa BWANA alitoka, akaua watu elfu mia moja na themanini na tano katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.


Nizitanguaye ishara za waongo, na kuwatia waganga wazimu; niwarudishaye nyuma wenye hekima, na kuyageuza maarifa yao kuwa ujinga;


Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.


Kuhusu Edomu. BWANA wa majeshi asema hivi, Je! Hakuna tena hekima katika Temani? Mashauri yamewapotea wenye busara? Je! Imetoweka hekima yao?


Mwasemaje, Sisi tuna akili, na Torati ya BWANA tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Siku hiyo, je! Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima cha Esau? Asema BWANA.


Ndipo Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua hakika kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.


Basi Daudi na watu wake, ambao walikuwa kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda popote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akauacha mpango wake.