Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 5:11 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huwainua juu walio wanyonge, wenye kuomboleza huwapa usalama.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huwainua juu walio wanyonge, wenye kuomboleza huwapa usalama.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huwainua juu walio wanyonge, wenye kuomboleza huwapa usalama.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Huwainua juu wanyonge, nao wale wanaoomboleza huinuliwa wakawa salama.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 5:11
15 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.


Yeye hawaondolei macho yake wenye haki; Lakini pamoja na wafalme huwaweka Katika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.


Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.


Lakini alimwinua mhitaji juu mbali na mateso, Na kuwaongeza jamaa zao kama kundi la kondoo.


Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.


Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.


Na miti yote ya mashamba itajua ya kuwa mimi, BWANA, nimeushusha chini mti mrefu, na kuuinua mti mfupi, na kuukausha mti mbichi, na kuusitawisha mti mkavu; mimi, BWANA, nimenena, nami nimelitenda jambo hili.


Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba. Heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka.


Mungu wa milele ndiye makazi yako, Na mikono ya milele i chini yako. Na mbele yako amemsukumia mbali adui; Akasema, Angamiza.


Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa;


Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu;


Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawaimarisha, atawathibitisha, atawatia nguvu na kuwapa msingi imara.