Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 5:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huinyeshea nchi mvua, hupeleka maji mashambani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huinyeshea nchi mvua, hupeleka maji mashambani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huinyeshea nchi mvua, hupeleka maji mashambani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 5:10
13 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa umeme wa radi.


Maana yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka ukungu wake;


Ambayo mawingu yainyesha Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.


Kwa kuwa huiambia theluji, Anguka juu ya nchi; Na pia kwa manyunyu ya mvua, Hayo manyunyu ya mvua yake nyingi.


Huzifunika mbingu kwa mawingu, Huitengenezea nchi mvua, Na kuichipusha nyasi milimani.


Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.


Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake.


Je! Katika vitu vya ubatili vya mataifa, kiko kitu kiwezacho kuleta mvua? Je! Mbingu zaweza kutoa manyunyu? Je! Si wewe, Ee BWANA, Mungu wetu? Kwa sababu hiyo tutakungoja; kwa kuwa wewe umevifanya vitu hivi vyote.


Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche BWANA, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea majuma ya mavuno yaliyoamriwa.


Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikauka.


Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.