Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 35:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwa sababu ya wingi wa dhuluma wao hulia; Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Kwa sababu ya udhalimu mwingi watu hulia, huomba msaada kwa sababu ya mapigo ya wenye nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Kwa sababu ya udhalimu mwingi watu hulia, huomba msaada kwa sababu ya mapigo ya wenye nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Kwa sababu ya udhalimu mwingi watu hulia, huomba msaada kwa sababu ya mapigo ya wenye nguvu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa sababu ya wingi wa dhuluma wao hulia; Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 35:9
20 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye huwaondoa makuhani wakiwa wamevuliwa nguo. Na kuwapindua mashujaa.


Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini; Amenyang'anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.


Watu huugua toka mji ulio na watu wengi, Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele; Wala Mungu hauangalii upumbavu.


Hata wakafanya kilio cha maskini kumfikia, Naye akasikia kilio cha hao wateswao.


Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.


Au je! Wewe una mkono kama Mungu? Waweza kutoa ngurumo kwa sauti kama yeye?


Uuvunje mkono wa mdhalimu, Na mwovu, uipatilize dhuluma yake, hadi usiione.


Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema BWANA, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.


Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?


Na kisha baada ya muda, yule mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa.


Ukiwatesa watu hao katika neno lolote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao,


BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;


Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.


Kisha nikarudi na kuona udhalimu wote unaotendeka chini ya jua; na tazama, machozi yao waliodhulumiwa, ambao walikuwa hawana mfariji; na upande wa wale waliowadhulumu kulikuwa na uwezo, lakini wale walikuwa hawana mfariji.


Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.


mpe ujira wake kwa siku yake, wala jua lisichwe juu yake; kwa maana ni maskini, moyo wake umeutumainia huo; asije akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako.