Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 32:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu; Wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Sitampendelea mtu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mtu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Sitampendelea mtu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mtu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Sitampendelea mtu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mtu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu; Wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 32:21
18 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo mimi mjakazi wako nikasema, Neno la bwana wangu mfalme na liwe la kustarehesha; kwa kuwa kama malaika wa Mungu ndivyo alivyo bwana wangu mfalme, kuyapambanua yaliyo mema na yaliyo mabaya; naye BWANA, Mungu wako na awe pamoja nawe.


mtumishi wako Yoabu ameyatenda haya ili kubadili uso wa jambo hili; na bwana wangu anayo akili, kama akili ya malaika wa Mungu, hata ajue mambo yote ya duniani.


Hakika atawakemea ninyi, Mkiwapendelea watu kwa siri.


Je! Mtamwonesha yeye upendeleo? Mtamtetea Mungu?


Nitanena, ili nipate kutulia; Nitafunua midomo yangu na kujibu.


Kwa kuwa mimi sijui kujipendekeza; Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.


Maneno yangu yatatamka uelekevu wa moyo wangu; Na hayo niyajuayo midomo yangu itayanena kwa unyofu.


Sembuse yeye huwajali nyuso za wakuu, Wala hawajali matajiri kuliko maskini? Kwani wote ni kazi ya mikono yake,


Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?


Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili. Kupendelea watu katika hukumu si kwema.


Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.


Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki.


Kwa sababu hiyo mimi nami nimewafanya ninyi kuwa kitu cha kudharauliwa, na unyonge, mbele ya watu wote, kama vile ninyi msivyozishika njia zangu, bali mmewapendelea watu katika sheria.


Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, tunajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.


Msitazame nafsi za watu katika hukumu; muwasikize wadogo na wakubwa sawasawa; msiche uso wa mtu yeyote; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu; na lile neno liwashindalo mniletee mimi, nami nitalisikiza.


Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.