Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi baba yake; na Rehoboamu mwanawe akatawala mahali pake.
Yobu 3:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni; Matoleo zaidiBiblia Habari Njema pamoja na wafalme na watawala wa dunia, waliojijengea upya magofu yao; Biblia Habari Njema - BHND pamoja na wafalme na watawala wa dunia, waliojijengea upya magofu yao; Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza pamoja na wafalme na watawala wa dunia, waliojijengea upya magofu yao; Neno: Bibilia Takatifu pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu, Neno: Maandiko Matakatifu pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu, BIBLIA KISWAHILI Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni; |
Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi baba yake; na Rehoboamu mwanawe akatawala mahali pake.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wamevuliwa nguo, Naye huwafanya waamuzi kuwa ni wapumbavu.
Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa, Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye, Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
Kwani najua kuwa utanileta hata kifoni, Niifikie nyumba waliyoaandaliwa wenye uhai wote.
Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na kifo kitakuwa mchungaji wao; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Miili yao itaoza, kao lao ni kuzimu.
Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu?
Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; Wala hakuna kuponyoka katika vita vile; Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.
Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;
Unafanyaje hapa? Nawe una nani hapa? Hata ukachimba kaburi hapa; ukamchimbia kaburi huko juu, na kumchongea makao katika jabali!
Ole wao waongezao nyumba baada ya nyumba, na kuweka shamba karibu na shamba, hadi ikawa hapana nafasi tena, nanyi ikawa hamna budi kukaa peke yenu katikati ya nchi!
Na watu wako watapajenga mahali palipokuwa ukiwa; utaiinua misingi ya vizazi vingi; nawe utaitwa, Mwenye kutengeneza mahali palipobomoka; na, Mwenye kurejesha njia za kukaa.
ndipo nitakapokushusha pamoja nao washukao shimoni, uende kwa watu wa kale; nami nitakukalisha pande za chini za nchi; mahali palipokuwa ukiwa tangu zamani, pamoja nao washukao shimoni; ili usikaliwe na watu, wala usiweke utukufu wako katika nchi yao walio hai.