Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 24:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huwasukuma maskini kando ya barabara; maskini wa dunia hujificha mbele yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huwasukuma maskini kando ya barabara; maskini wa dunia hujificha mbele yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huwasukuma maskini kando ya barabara; maskini wa dunia hujificha mbele yao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 24:4
22 Marejeleo ya Msalaba  

Mwuaji huamka asubuhi kukipambazuka, huwaua maskini na wahitaji; Tena wakati wa usiku yu kama mwizi.


Kwa sababu nilimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.


Nilikuwa baba kwa mhitaji, Na kesi ya mtu nisiyemjua niliichunguza.


Je! Mimi sikulia kwa ajili ya huyo aliyekuwa katika taabu? Nafsi yangu, je! Haikusononeka kwa ajili ya wahitaji?


Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;


Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo, Au wahitaji kukosa mavazi;


Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili, Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, Hata akamwua mtu aliyevunjika moyo,


Heri amkumbukaye mnyonge; BWANA atamwokoa siku ya taabu.


Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.


Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara.


Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi; Bali waovu waondokapo, watu hujificha.


Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.


Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.


ili kumpotosha mhitaji asipate haki yake, na kuwanyang'anya maskini wa watu wangu haki yao; ili wajane wawe mateka yao, na kuwafanya yatima waliofiwa na baba zao kuwa mawindo yao!


na kuwadhulumu maskini na wahitaji, na kuwanyang'anya watu mali yao kwa nguvu, wala hakurudisha rehani, naye ameviinulia macho vinyago, na kufanya machukizo,


Kwa habari za yule baba yake, kwa sababu aliwaonea watu kwa ukali mwingi, na kumnyang'anya ndugu yake mali yake kwa nguvu; na kuyatenda yasiyo mema kati ya watu wake, tazama, atakufa katika uovu wake.


Watu wa nchi wametumia udhalimu, wamenyang'anya kwa nguvu; naam, wamewatenda jeuri maskini na wahitaji, nao wamewaonea wageni bila haki.


nao hukanyaga vichwa vya maskini katika mavumbi ya nchi na kuwasukuma walioteseka kutoka kwa njia yao; na mtu na baba yake wanamwendea mwanamke mmoja, na kulitia unajisi jina langu takatifu;


Lisikieni neno hili, enyi ng'ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao, Haya! Leteni, tunywe.