Basi, mfalme akiona vema, na iandikwe kwamba waangamizwe; nami nitalipa talanta elfu kumi za fedha mikononi mwa watakaosimamia shughuli hiyo, waziweke katika hazina ya mfalme.
Yobu 18:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe, Naye huenda juu ya matanzi. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni; kila akitembea anakumbana na shimo. Biblia Habari Njema - BHND Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni; kila akitembea anakumbana na shimo. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni; kila akitembea anakumbana na shimo. Neno: Bibilia Takatifu Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu. Neno: Maandiko Matakatifu Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu. BIBLIA KISWAHILI Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe, Naye huenda juu ya matanzi. |
Basi, mfalme akiona vema, na iandikwe kwamba waangamizwe; nami nitalipa talanta elfu kumi za fedha mikononi mwa watakaosimamia shughuli hiyo, waziweke katika hazina ya mfalme.
Basi Hamani akawasimulia Zereshi mkewe na marafiki zake wote kila neno lililompata. Kisha watu wake wenye hekima na Zereshi mkewe wakamwambia, Ikiwa huyu Mordekai, ambaye umeanza kuanguka mbele yake, ni wa uzao wa Wayahudi, wewe hutamweza, bali kuanguka utaanguka mbele yake.
Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.
Ndipo mfalme Ahasuero aliponena, akamwambia malkia Esta, Ni nani huyu, tena yuko wapi, ambaye moyoni mwake alithubutu kufanya hivi?
Mavuno yake wale wenye njaa huyala, Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani, Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.
Uharibifu na umpate kwa ghafla, Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; Kwa uharibifu aanguke ndani yake.
Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika.
Bwana MUNGU asema hivi; Nitautanda wavu wangu juu yako, kwa kusanyiko la watu wa kabila nyingi; nao watakuvua katika jarife langu.
Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na mtego, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, zinazowaingiza watu katika upotevu na uharibifu.
wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambaye amewanasa, hata wakayafanya mapenzi yake.