Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 18:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nchini hakuna atakayemkumbuka; jina lake halitatamkwa tena barabarani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nchini hakuna atakayemkumbuka; jina lake halitatamkwa tena barabarani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nchini hakuna atakayemkumbuka; jina lake halitatamkwa tena barabarani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 18:17
13 Marejeleo ya Msalaba  

Maneno yenu ya hekima ni mithali ya majivu, Ngome zenu ni ngome za udongo.


Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.


Wazawa wake waangamizwe, Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.


Ziwe mbele za BWANA daima, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.


Uso wa BWANA ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.


Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya, Atakufa lini, jina lake lipotee?


Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.


Adui wameangamia na kuwa magofu milele. Nayo miji yao uliing'oa; Hata kumbukumbu lao limepotea.


Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka; Bali jina la mtu mwovu litaoza.


Bali waovu watatengwa na nchi, Nao wafanyao hila watang'olewa.


Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi, Kwa maana umeiharibu nchi yako, Umewaua watu wako; Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele.


Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao.


Tena BWANA ametoa amri katika habari zako, ya kwamba asiwepo tena mtu awaye yote mwenye jina lako; toka nyumba ya miungu yako nitakatilia mbali sanamu ya kuchora, na sanamu ya kuyeyusha; nitakufanyia kaburi lako; kwa maana u mbovu.