Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 13:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa; nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa; nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa; nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 13:4
23 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo mimi nikatuma kwake wajumbe, kusema, Hakukufanyika mambo kama hayo uyasemayo, lakini kwa moyo wako wewe mwenyewe umeyabuni.


Nimesikia maneno mengi mfano wa hayo; Ninyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha.


Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe; Mbona basi mmebatilika kabisa?


Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.


Wameudhika kwa sababu walitumaini; Wakaja huku, nao walifadhaika.


Kwani sasa ninyi mmekuwa hivyo; Mnaona maafa yangu, na kuogopa.


Wenye kiburi wamenizulia uongo, Lakini kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.


Usimshuhudie jirani yako uongo.


Tazama, mimi niko juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA.


Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha lako huna dawa ziponyazo.


Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.


Wameliponya jeraha la watu wangu kwa juu juu tu, wakisema, Amani, Amani, wala hapana amani.


Je! Hakuna marhamu katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu?


Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.


Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha lake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha lenu.


Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.


na kuvumilia mateso mengi kutoka kwa matabibu wengi, na kugharimiwa mali yake yote aliyokuwa nayo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.