Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 11:11 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwa kuwa yeye awajua watu baradhuli; Anapouona uovu, je; hatauangalia?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mungu anajua watu wasiofaa; akiona maovu yeye huchukua hatua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mungu anajua watu wasiofaa; akiona maovu yeye huchukua hatua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mungu anajua watu wasiofaa; akiona maovu yeye huchukua hatua.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa kuwa yeye awajua watu baradhuli; Anapouona uovu, je; hatauangalia?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 11:11
17 Marejeleo ya Msalaba  

Huwapa usalama, nao wapumzika kwao; Na macho yake yako juu ya njia zao.


Maana anatazama hata miisho ya nchi, Na kuona chini ya mbingu nzima.


Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?


Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, Auficha uso wake, haoni kamwe.


Umeona, maana unaangalia matatizo na dhiki, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.


Toka mbinguni BWANA huchungulia, Huangalia na kuwaona wanadamu wote.


Wewe, BWANA, umeona, usinyamaze; Ee Bwana, usiwe mbali nami.


BWANA anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.


Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu, Aliye Juu kuliko walio juu huangalia; Tena wako walio juu kupita hao.


Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu.


Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;


Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, maana vitu vyote ni tupu na kuwekwa wazi machoni pake yeye ambaye tunapaswa kuwajibika kwake.


nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye fikira na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.