Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 46:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Misri ni mtamba mzuri sana, lakini uharibifu umekuja, Umekuja utokao pande za kaskazini.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Misri ni kama mtamba mzuri wa ng'ombe, lakini kipanga kutoka kaskazini amemvamia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Misri ni kama mtamba mzuri wa ng'ombe, lakini kipanga kutoka kaskazini amemvamia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Misri ni kama mtamba mzuri wa ng'ombe, lakini kipanga kutoka kaskazini amemvamia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Misri ni mtamba mzuri, lakini mbung’o anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Misri ni mtamba mzuri sana, lakini uharibifu umekuja, Umekuja utokao pande za kaskazini.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 46:20
8 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo BWANA akaniambia, Toka kaskazini mabaya yatatokea, na kuwapata watu wote wakaao katika nchi hii.


angalieni, nitatuma watu na kuzitwaa jamaa zote za upande wa kaskazini, asema BWANA, nami nitatuma ujumbe kwa Nebukadneza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitawaleta juu ya nchi hii, na juu yao wakaao ndani yake, na juu ya mataifa haya yote yaliyoko pande zote; nami nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kitu cha kushangaza, na kitu cha kuzomewa, na ukiwa wa daima.


Maana hiyo ni siku ya Bwana, BWANA wa majeshi, Siku ya kisasi, ili ajilipize kisasi juu ya adui zake; Nao upanga utakula na kushiba, Utakunywa damu yao hata kukinai; Maana Bwana, BWANA wa majeshi, ana sadaka yake Katika nchi ya kaskazini karibu na mto Frati.


Binti ya Misri ataaibishwa; Atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.


Mtu mwepesi asikimbie, wala shujaa asiokoke; pande za kaskazini karibu na mto Frati wamejikwaa na kuanguka.


BWANA asema hivi, Tazama, maji yanatokea katika pande za kaskazini, nayo yatakuwa mto ufurikao, nayo yataifunika nchi, na kila kitu kilichomo, huo mji na wote wakaao ndani yake; nao watu watalia na watu wote wakaao katika nchi wataomboleza.


Kwa sababu mnafurahi, kwa sababu mnashangilia, enyi mnaouteka urithi wangu, kwa sababu mmenona kama mtamba akanyagaye nafaka, nanyi mnalia kama farasi wenye nguvu;


Naye Efraimu ni ndama aliyefundishwa, apendaye kupura; lakini nimepitisha kongwa juu ya shingo yake nzuri; nitampandisha mwenye kupanda juu ya Efraimu; Yuda atalima, na Yakobo atapiga haro yeye mwenyewe.