Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 46:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mataifa wamesikia habari za aibu yako, nayo dunia imejaa kilio chako; maana shujaa amejikwaa juu ya shujaa mwenzake, wameanguka wote wawili pamoja.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mataifa yamesikia aibu yenu, kilio chenu kimeenea duniani kote; mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe, wote pamoja wameanguka.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mataifa yamesikia aibu yenu, kilio chenu kimeenea duniani kote; mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe, wote pamoja wameanguka.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mataifa yamesikia aibu yenu, kilio chenu kimeenea duniani kote; mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe, wote pamoja wameanguka.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mataifa wamesikia habari za aibu yako, nayo dunia imejaa kilio chako; maana shujaa amejikwaa juu ya shujaa mwenzake, wameanguka wote wawili pamoja.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 46:12
17 Marejeleo ya Msalaba  

Watainama chini ya wafungwa tu, wataanguka chini yao waliouawa. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


Nami nitawaamsha Wamisri juu ya Wamisri; nao watapigana, kila mtu na ndugu yake, na kila mtu na jirani yake, mji juu ya mji, na ufalme juu ya ufalme.


Pana kilio katika njia kuu kwa sababu ya divai; furaha yote imetiwa giza, na changamko la nchi limetoweka.


Yuda huomboleza, Na malango yake yamelegea; Wameketi chini wamevaa kaniki; Na kilio cha Yerusalemu kimepaa juu.


Mbona unatangatanga hivi upate kugeuza mwendo wako? Utaona haya kwa ajili ya Misri pia, kama ulivyoona haya kwa ajili ya Ashuru.


Mtu mwepesi asikimbie, wala shujaa asiokoke; pande za kaskazini karibu na mto Frati wamejikwaa na kuanguka.


BWANA asema hivi, Tazama, maji yanatokea katika pande za kaskazini, nayo yatakuwa mto ufurikao, nayo yataifunika nchi, na kila kitu kilichomo, huo mji na wote wakaao ndani yake; nao watu watalia na watu wote wakaao katika nchi wataomboleza.


Toka kilio cha Heshboni mpaka Eleale, naam, mpaka Yahasa, wametoa sauti zao, toka Soari mpaka Horonaimu, hata Eglath-shelishia; maana maji ya Nimrimu nayo yatakuwa ukiwa.


Nchi yatetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao; Kuna kilio, sauti yake yasikiwa katika Bahari ya Shamu.


Kwa kishindo cha kutwaliwa Babeli nchi itatetemeka, Na kilio chake chasikiwa katika mataifa.


Sauti ya kilio kutoka Babeli, Na ya uangamizi mkuu toka nchi ya Wakaldayo!


Awakumbuka watu wake wenye heshima; Wanajikwaa katika mwendo wao; Wanafanya haraka waende ukutani; Nacho kitu cha kuwafunika kimetayarishwa.


Na katika siku ile, asema BWANA kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani.


Na wale wasiokufa walipigwa kwa yale majipu; na kilio cha mji kikafika mbinguni.