Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 45:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ulisema, Ole wangu! Kwa maana BWANA ameongeza huzuni pamoja na maumivu yangu. Nimechoka kwa ajili ya kuugua kwangu, wala sioni raha.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wewe ulisema, ‘Ole wangu! Mwenyezi-Mungu ameniongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka kupiga kite, wala sipati pumziko.’

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wewe ulisema, ‘Ole wangu! Mwenyezi-Mungu ameniongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka kupiga kite, wala sipati pumziko.’

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wewe ulisema, ‘Ole wangu! Mwenyezi-Mungu ameniongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka kupiga kite, wala sipati pumziko.’

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ulisema, ‘Ole wangu! Mwenyezi Mungu ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’ ”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ulisema, ‘Ole wangu! bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’ ”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ulisema, Ole wangu! Kwa maana BWANA ameongeza huzuni pamoja na maumivu yangu. Nimechoka kwa ajili ya kuugua kwangu, wala sioni raha.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 45:3
28 Marejeleo ya Msalaba  

Hata leo malalamiko yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu.


Ole wangu mimi! Kwa kuwa ni mgeni katika Mesheki; Na kufanya makao yangu Katikati ya hema za Kedari.


Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA Katika nchi ya walio hai.


Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maporomoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.


Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakibubujikia kitanda changu; Nililowesha godoro langu kwa machozi yangu.


Macho yangu yameharibika kwa masumbufu, Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.


Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofika Kwa kumngoja Mungu wangu.


Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.


BWANA, Mungu wa Israeli, akuambia wewe Ee Baruku;


Laiti ningeweza kujifariji, nisione huzuni! Moyo wangu umezimia ndani yangu.


Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu kuwa chemchemi ya machozi, ili nipate kulia mchana na usiku kwa ajili yao waliouawa wa binti ya watu wangu!


Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu, Nao umeishinda; Ametandika wavu aninase miguu, Amenirudisha nyuma; Amenifanya kuwa mtu wa pekee, Na mgonjwa mchana kutwa.


Huo uovu wao wote Na uje mbele zako wewe; Ukawatende wao kama ulivyonitenda mimi Kwa dhambi zangu zote; Kwa maana mauguzi yangu ni mengi sana, Na moyo wangu umezimia.


Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.


Kwa sababu hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii, kwa jinsi tulivyopata rehema, hatulegei;


Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.


Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.


Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.