Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 4:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Niione bendera hata lini, na kuisikia sauti ya tarumbeta?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hadi lini nitaona bendera ya vita na kuisikia sauti ya tarumbeta?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hadi lini nitaona bendera ya vita na kuisikia sauti ya tarumbeta?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hadi lini nitaona bendera ya vita na kuisikia sauti ya tarumbeta?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Niione bendera hata lini, na kuisikia sauti ya tarumbeta?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 4:21
11 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote wanaume kwa wawanawake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hadi leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika Maombolezo.


Mwaka ulipokwisha, Nebukadneza akatuma wajumbe, akamchukua mpaka Babeli; pamoja na vyombo vya thamani vya nyumba ya BWANA; akamtawaza Sedekia nduguye awe mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu.


Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mnyonge; akawatia wote mkononi mwake.


Naye mfalme wa Misri akamwondoa katika Yerusalemu, akaitoza nchi talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu.


Mtima wangu, mtima wangu! Naumwa katika moyo wangu wa ndani; moyo wangu umefadhaika ndani yangu; siwezi kunyamaza; kwa sababu umesikia, Ee nafsi yangu, sauti ya tarumbeta, mshindo wa vita.


Uangamivu baada ya uangamivu umetangazwa; kwa maana nchi yote imeharibika; hema zangu zimetekwa nyara ghafla, na mapazia yangu katika dakika moja.


Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.


mkisema, La! Lakini tutakwenda nchi ya Misri, ambayo hatutaona vita, wala kuisikia sauti ya tarumbeta, wala kuona njaa kwa kukosa chakula; nasi tutakaa huko;


Kimbieni mpate kuwa salama, enyi wana wa Benyamini; tokeni katika Yerusalemu, pigeni tarumbeta katika Tekoa, simamisheni ishara juu ya Beth-hakeremu; kwa maana mabaya yanachungulia toka kaskazini, na uharibifu mkuu.