Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 37:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na Wakaldayo watakuja tena, na kupigana na mji huu; nao watautwaa, na kuuteketeza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Na Wakaldayo watarudi kuushambulia mji huu. Watauteka mji na kuuteketeza kwa moto.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Na Wakaldayo watarudi kuushambulia mji huu. Watauteka mji na kuuteketeza kwa moto.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Na Wakaldayo watarudi kuushambulia mji huu. Watauteka mji na kuuteketeza kwa moto.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na Wakaldayo watakuja tena, na kupigana na mji huu; nao watautwaa, na kuuteketeza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 37:8
9 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Angalieni, nitazigeuza nyuma silaha za vita zilizo mikononi mwenu, ambazo kwa hizo ninyi mnapigana na mfalme wa Babeli, na Wakaldayo, wanaowahusuru nje ya kuta zenu, nami nitazikusanya pamoja katikati ya mji huu.


na Wakaldayo, wanaopigana na mji huu, watakuja, na kuutia moto mji huu, na kuuteketeza, pamoja na nyumba zake, ambazo juu ya madari yake wamemfukizia Baali uvumba, na kuwamiminia miungu mingine vinywaji, ili kunikasirisha.


BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nenda ukaseme na Sedekia, mfalme wa Yuda, ukamwambie, BWANA asema hivi, Tazama, nitatia mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto;


Maana mngelipiga jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi, wakabaki kati yao watu waliojeruhiwa tu, hata hivyo wangeondoka kila mtu katika hema yake, na kuuteketeza mji huu.


bali ukikataa kutoka kwenda kwa wakuu wa mfalme wa Babeli, basi, mji huu utatiwa katika mikono ya Wakaldayo nao watauteketeza, hata na wewe hutajiepusha na mikono yao.


Na watawatoa wake zako, na watoto wako wote, na kuwachukua kwa Wakaldayo; wala wewe hutapona na mikono yao, bali utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babeli, nawe utakuwa sababu ya kuteketezwa mji huu.


BWANA asema hivi, Bila shaka mji huu utatiwa katika mikono ya jeshi la mfalme wa Babeli, naye atautwaa.