Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 30:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana BWANA asema hivi, Maumivu yako hayaponyeki, na jeraha lako ni kubwa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Majeraha yako hayaponyeki, vidonda vyako havitibiki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Majeraha yako hayaponyeki, vidonda vyako havitibiki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Majeraha yako hayaponyeki, vidonda vyako havitibiki.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “ ‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Hili ndilo asemalo bwana: “ ‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana BWANA asema hivi, Maumivu yako hayaponyeki, na jeraha lako ni kubwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 30:12
13 Marejeleo ya Msalaba  

lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.


Nawe utawaambia neno hili, Macho yangu na yatiririke machozi, usiku na mchana, wala yasikome; kwa maana bikira, binti ya watu wangu, amevunjika mavunjiko makuu, kwa jeraha lisiloponyeka.


Je! Umemkataa Yuda kabisa? Roho yako imeichukia Sayuni? Mbona umetupiga, tusiwe na dawa ya kutuponya? Tulitazamia amani, lakini hayakuja mema yoyote, tulitazamia wakati wa kupona, na tazama, kufadhaika tu!


Mbona maumivu yangu ni ya daima, na jeraha langu halina dawa, linakataa kuponywa? Je! Yamkini wewe utakuwa kwangu kama kijito kidanganyacho, na kama maji yasiyodumu?


Mbona unalilia maumivu yako? Maumivu yako hayaponyeki; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya.


Kama vile kisima kitoavyo maji yake, ndivyo utoavyo uovu wake; jeuri na kuharibu kwasikiwa ndani yake; ugonjwa na jeraha zi mbele zangu daima.


Je! Hakuna marhamu katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu?


Nikushuhudie nini? Nikufananishe na nini, Ee Binti Yerusalemu? Nikulinganishe na nini, nipate kukufariji, Ee bikira binti Sayuni? Kwa maana uvunjifu wako ni mkuu kama bahari, Ni nani awezaye kukuponya?


Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.


Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha lake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha lenu.


Kwa maana majeraha yake hayaponyeki; Maana msiba umeijia hata Yuda, Unalifikia lango la watu wangu, Naam, hata Yerusalemu.


Jeraha lako halipunguziki; donda lako haliponyeki; wote wasikiao habari zako wapiga makofi juu yako; kwa maana ni nani aliyewahi kuukwepa ukatili wako usio na mwisho?