Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 17:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huyo ni kama kichaka jangwani, hataona chochote chema kikimjia. Ataishi mahali pakavu nyikani, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huyo ni kama kichaka jangwani, hataona chochote chema kikimjia. Ataishi mahali pakavu nyikani, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huyo ni kama kichaka jangwani, hataona chochote chema kikimjia. Ataishi mahali pakavu nyikani, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 17:6
17 Marejeleo ya Msalaba  

Basi yule afisa, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama BWANA angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.


Hataiangalia hiyo mito ya maji, Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.


Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake, Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.


Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.


Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi, Kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.


Hata wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakastawi. Mwishowe wataangamizwa milele;


Maana mtakuwa kama mwaloni ambao majani yake yakauka, na kama bustani isiyo na maji.


basi, BWANA asema hivi, Tazama, nitamwadhibu Shemaya, Mnehelami, na wazawa wake; hatakuwa na mtu atakayekaa katika watu hawa, wala hatayaona mema nitakayowatendea watu wangu, asema BWANA; kwa sababu amenena maneno ya uasi juu ya BWANA.


Haya! Kimbieni! Jiokoeni nafsi zenu! Mkawe kama mtu aliye mkiwa.


Bali mahali penye matope, na maziwa yake, hayataponywa; yataachwa yawe ya chumvi.


Basi kama niishivyo, asema BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, Hakika Moabu atakuwa kama Sodoma, na wana wa Amoni kama Gomora, yaani, milki ya upupu, na mashimo ya chumvi, ukiwa wa daima; watu wangu waliosalia watawateka nyara, na watu wa taifa langu waliobaki watawarithi.


ya kuwa nchi yake nzima ni kibiriti, na chumvi, na kuteketea, haipandwi, wala haizai, wala nyasi hazimei humo, kama mapinduko ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, aliyoipindua BWANA kwa ghadhabu yake na hasira zake;


Abimeleki akapigana na huo mji mchana kutwa; akautwaa mji, akawaua watu waliokuwamo ndani yake; kisha akauteketeza mji, na kuutia chumvi.