Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yeremia 12:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Umewapanda, naam, wametia mizizi, wanakua, naam, wanazaa matunda; katika vinywa vyao u karibu, bali katika mioyo yao u mbali.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Unawaotesha nao wanaota; wanakua na kuzaa matunda. Wanakutaja kwa maneno yao, lakini mioyo yao iko mbali nawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Unawaotesha nao wanaota; wanakua na kuzaa matunda. Wanakutaja kwa maneno yao, lakini mioyo yao iko mbali nawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Unawaotesha nao wanaota; wanakua na kuzaa matunda. Wanakutaja kwa maneno yao, lakini mioyo yao iko mbali nawe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Umewapanda, naam, wametia mizizi, wanakua, naam, wanazaa matunda; katika vinywa vyao u karibu, bali katika mioyo yao u mbali.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yeremia 12:2
15 Marejeleo ya Msalaba  

Watu huugua toka mji ulio na watu wengi, Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele; Wala Mungu hauangalii upumbavu.


Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake.


Nimemwona mtu asiye haki mkali sana, Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni.


Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walichonacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;


Kwa maana BWANA wa majeshi, aliyekupanda, ametamka mabaya juu yako, kwa sababu ya maovu ya nyumba ya Israeli, na ya nyumba ya Yuda, waliyoyatenda juu ya nafsi zao wenyewe kwa kunikasirisha, wakimfukizia Baali uvumba.


Na pamoja na hayo yote dada yake, Yuda mwenye hiana, hajanirudia mimi kwa moyo wake wote, bali kwa unafiki, asema BWANA.


Basi, mwambie hivi, BWANA asema hivi, Tazama, niliyoyajenga nitayabomoa, na niliyoyapanda nitayang'oa; na haya yatakuwa katika nchi yote.


Nao huja kwako kama watu wajavyo, nao hukaa mbele yako kama watu wangu, nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao.


Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.


Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;


Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.


Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa huniheshimu kwa midomo Ila mioyo yao iko mbali nami;


Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala hawafai kwa tendo lolote jema.