Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wimbo Ulio Bora 4:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Amka, kaskazi; nawe uje, kusi; Vumeni juu ya bustani yangu, Manukato ya bustani yatokee. Mpendwa wangu na aingie bustanini mwake, Akayale matunda yake mazuri.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Vuma, ewe upepo wa kaskazi, njoo, ewe upepo wa kusi; vumeni juu ya bustani yangu, mlijaze anga kwa manukato yake. Mpenzi wangu na aje bustanini mwake, ale matunda yake bora kuliko yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Vuma, ewe upepo wa kaskazi, njoo, ewe upepo wa kusi; vumeni juu ya bustani yangu, mlijaze anga kwa manukato yake. Mpenzi wangu na aje bustanini mwake, ale matunda yake bora kuliko yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Vuma, ewe upepo wa kaskazi, njoo, ewe upepo wa kusi; vumeni juu ya bustani yangu, mlijaze anga kwa manukato yake. Mpenzi wangu na aje bustanini mwake, ale matunda yake bora kuliko yote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Amka, upepo wa kaskazini, na uje, upepo wa kusini! Vuma juu ya bustani yangu, ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ng’ambo. Mpenzi wangu na aje bustanini mwake na kuonja matunda mazuri sana.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Amka, upepo wa kaskazini, na uje, upepo wa kusini! Vuma juu ya bustani yangu, ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ng’ambo. Mpendwa wangu na aje bustanini mwake na kuonja matunda mazuri sana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Amka, kaskazi; nawe uje, kusi; Vumeni juu ya bustani yangu, Manukato ya bustani yatokee. Mpendwa wangu na aingie bustanini mwake, Akayale matunda yake mazuri.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wimbo Ulio Bora 4:16
30 Marejeleo ya Msalaba  

Upepo huvuma kuelekea kusini, kisha huvuma kuelekea kaskazini; hugeuka daima katika mwendo wake, nao huyarudia mazunguko yake.


nikajifanyia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;


Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu.


Nivute nyuma yako, na tukimbie; Mfalme ameniingiza vyumbani mwake. Tutafurahi na kukushangilia; Tutalinena pendo lako kuliko divai; Ndiyo, ina haki wakupende.


Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Niliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake niliyaonja kuwa matamu.


Sikiliza! Ni mpendwa wangu! Tazama, anakuja, Akiruka milimani, akichachawa vilimani.


Naingia bustanini mwangu, dada yangu, bibi arusi, Nachuma manemane yangu na rihani, Nala sega la asali na asali yangu, Nanywa divai yangu na maziwa. Kaleni, rafiki zangu, kanyweni, Naam, nyweni sana, wapendwa wangu.


Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro.


Shamba langu la mizabibu, lililo langu mimi, liko mbele yangu. Basi, Sulemani, wewe uwe na elfu zako, Na hao wayalindao matunda yake wapewe mia mbili.


Laiti ungepasua mbingu, na kushuka, ili milima itetemeke mbele zako;


Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapulizie hawa waliouawa, wapate kuishi.


Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi.


Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.


Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.


Yesu akamwambia, Simama, jitwike godoro lako, uende.


Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.


ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa, niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.


Basi nikiisha kuimaliza kazi hiyo, na kuwatilia mhuri tunda hilo, nitapitia kwenu, kwenda Spania.


Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa muwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.


Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.