Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wimbo Ulio Bora 3:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wote wameshika upanga, Wamehitimu kupigana; Kila mtu anao upanga wake pajani Kwa hofu ya kamsa za usiku.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kila mmoja wao ameshika upanga, kila mmoja wao ni hodari wa vita. Kila mmoja ana upanga wake mkononi, tayari kumkabili adui usiku.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kila mmoja wao ameshika upanga, kila mmoja wao ni hodari wa vita. Kila mmoja ana upanga wake mkononi, tayari kumkabili adui usiku.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kila mmoja wao ameshika upanga, kila mmoja wao ni hodari wa vita. Kila mmoja ana upanga wake mkononi, tayari kumkabili adui usiku.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya vitisho vya usiku.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wote wameshika upanga, Wamehitimu kupigana; Kila mtu anao upanga wake pajani Kwa hofu ya kamsa za usiku.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wimbo Ulio Bora 3:8
13 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa tokea wakati huo, nusu ya watumishi wangu walitumika katika kazi hiyo, na nusu yao wakaishika mikuki, na ngao, na pinde, na darii; na viongozi walikuwa nyuma ya nyumba yote ya Yuda.


Watu wale walioujenga ukuta, na wale waliochukua mizigo, walijitweka wenyewe, kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono wake wa pili alishika silaha yake;


Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako.


Hutaogopa hatari za usiku, Wala mshale urukao mchana,


Tazama, ni machela yake Sulemani; Mashujaa sitini waizunguka, Wa mashujaa wa Israeli.


Mfalme Sulemani alijitengenezea machela Ya miti ya Lebanoni;


Mimi, BWANA, nililinda, Nitalitia maji kila dakika, Asije mtu akaliharibu; Usiku na mchana nitalilinda.


Kwa maana juu ya Babeli nitaamsha na kuleta kusanyiko la mataifa makubwa, toka nchi ya kaskazini; nao watajipanga juu yake; kutoka huko atatwaliwa; mishale yao itakuwa kama ya mtu shujaa aliye stadi; hakuna hata mmoja utakaorudi bure.


Ehudi alijifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wake ulipata dhiraa moja; akaufunga huo upanga ndani ya nguo yake katika paja lake la mkono wa kulia.