Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wimbo Ulio Bora 3:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kitambo kidogo tu nilipoachana nao, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mara tu nilipoachana nao, nilimwona mpenzi wangu wa moyo; nikamshika wala sikumwachia aondoke, hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu, hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mara tu nilipoachana nao, nilimwona mpenzi wangu wa moyo; nikamshika wala sikumwachia aondoke, hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu, hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mara tu nilipoachana nao, nilimwona mpenzi wangu wa moyo; nikamshika wala sikumwachia aondoke, hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu, hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende hadi nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kitambo kidogo tu nilipoachana nao, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wimbo Ulio Bora 3:4
21 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.


Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.


Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.


Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu, Ni wapi utakapolisha kundi lako, Ni wapi utakapolilaza adhuhuri. Kwa nini niwe kama aliyefungiwa shela, Karibu na makundi ya wenzako?


Kabla sijajua, roho yangu ilinileta Katikati ya magari ya wakuu wangu.


Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli, Na nywele za kichwa chako kama urujuani, Mfalme amenaswa na mashungi yake.


Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu, Naye angenifundisha; Ningekunywesha divai iliyokolea, Divai mpya ya mkomamanga wangu.


Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, BWANA, nasema ukweli; nanena mambo ya haki.


Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.


BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.


Na tazama, Yesu akakutana nao, akisema, Salamu! Wakakaribia wakamshika miguu, wakamsujudia.


Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;


Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?


wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.


Bali Yerusalemu wa juu ni muungwana, naye ndiye mama yetu sisi.