Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wimbo Ulio Bora 3:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini, Katika njia zake na viwanjani, Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu. Nikamtafuta, nisimpate.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Niliamka nikazunguka mjini, barabarani na hata vichochoroni, nikimtafuta yule wangu wa moyo. Nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Niliamka nikazunguka mjini, barabarani na hata vichochoroni, nikimtafuta yule wangu wa moyo. Nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Niliamka nikazunguka mjini, barabarani na hata vichochoroni, nikimtafuta yule wangu wa moyo. Nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini, Katika njia zake na viwanjani, Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu. Nikamtafuta, nisimpate.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wimbo Ulio Bora 3:2
18 Marejeleo ya Msalaba  

Ana heri mtu yule anisikilizaye, Akisubiri sikuzote malangoni pangu, Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.


Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu, Ni wapi utakapolisha kundi lako, Ni wapi utakapolilaza adhuhuri. Kwa nini niwe kama aliyefungiwa shela, Karibu na makundi ya wenzako?


Walinzi wazungukao mjini waliniona; Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?


Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondosha manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo.


Tena hapana aliitiaye jina lako, ajitahidiye akushike; kwa kuwa umetuficha uso wako, nawe umetukomesha kwa njia ya maovu yetu.


Pigeni mbio huku na huku katika njia za Yerusalemu, mkaone sasa, na kujua, na kutafuta katika viwanja vyake, kwamba mwaweza kumpata mtu mmoja, kwamba yuko mtu mmoja awaye yote atendaye kwa haki, atafutaye uaminifu; nami nitausamehe mji huo.


Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.


Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini


Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.


Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.