Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wimbo Ulio Bora 3:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Usiku kitandani nilimtafuta mpendwa wa nafsi yangu, Nilimtafuta, nisimpate.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Usiku nikiwa kitandani mwangu, niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu; nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Usiku nikiwa kitandani mwangu, niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu; nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Usiku nikiwa kitandani mwangu, niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu; nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usiku kitandani nilimtafuta mpendwa wa nafsi yangu, Nilimtafuta, nisimpate.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wimbo Ulio Bora 3:1
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha.


Muwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.


Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakibubujikia kitanda changu; Nililowesha godoro langu kwa machozi yangu.


Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu, Ni wapi utakapolisha kundi lako, Ni wapi utakapolilaza adhuhuri. Kwa nini niwe kama aliyefungiwa shela, Karibu na makundi ya wenzako?


Nilimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.


Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Ninyi mkimwona mpendwa wangu, Ni nini mtakayomwambia? Ya kwamba nazimia kwa mapenzi.


Kwa nafsi yangu nimekutamani wakati wa usiku; Naam, kwa nafsi yangu ndani yangu nitakutafuta mapema; Maana hukumu zako zikiwapo duniani, Watu wakaao duniani hujifunza haki.


Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yuko karibu;


Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.


Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea.


Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.


Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamumwoni sasa, mnamwamini; na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu,