Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waroma 8:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mwenyezi Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waroma 8:14
24 Marejeleo ya Msalaba  

Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze katika njia iliyo sawa,


Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.


Tena itakuwa ya kwamba hesabu ya wana wa Israeli itafanana na mchanga wa bahari, usioweza kupimwa wala kuhesabiwa; tena itakuwa, badala ya kuambiwa, Ninyi si watu wangu, wataambiwa, Ninyi ndio wana wa Mungu aliye hai.


Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.


Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;


Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.


Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.


Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.


Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.


yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazawa.


Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike, asema Bwana Mwenyezi.


Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.


kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.


Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.


Basi nasema, Nendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.


Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.


Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, kulingana na radhi ya mapenzi yake.


kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;


Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.


Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.


Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.