Tena mwanamume akimtwaa mke wa nduguye, ni upotovu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana.
Walawi 18:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Kamwe usilale na mke wa ndugu yako; huyo ni shemeji yako. Biblia Habari Njema - BHND Kamwe usilale na mke wa ndugu yako; huyo ni shemeji yako. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Kamwe usilale na mke wa ndugu yako; huyo ni shemeji yako. Neno: Bibilia Takatifu “ ‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako. Neno: Maandiko Matakatifu “ ‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako. BIBLIA KISWAHILI Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo. |
Tena mwanamume akimtwaa mke wa nduguye, ni upotovu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana.
wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.
Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo, ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;
Lakini mfalme Herode alipokaripiwa na yeye kwa ajili ya Herodia, mke wa nduguye, na maovu yote aliyoyafanya Herode,
Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe.