Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wakolosai 3:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wakolosai 3:2
20 Marejeleo ya Msalaba  

Basi sasa jitieni moyo na nia kumtafuta BWANA, Mungu wenu; inukeni basi, mkamjengee BWANA Mungu mahali patakatifu, ili kulileta sanduku la Agano la BWANA, na vyombo vitakatifu vya Mungu, ndani ya nyumba itakayojengwa kwa ajili ya jina la BWANA.


Nami tena kwa kuwa nimeiwekea nyumba ya Mungu wangu shauku yangu, nami ninayo hazina yangu mwenyewe ya dhahabu na fedha, ninaitoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, zaidi ya hiyo akiba niliyoiwekea tayari nyumba takatifu;


Msiitumainie dhuluma, Wala msijivune kwa unyang'anyi; Mali izidipo msiiangalie sana moyoni.


Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.


Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu? Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa, Kama tai arukaye mbinguni.


Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lolote litakalofuata baada yake.


Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.


Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wezi huvunja na kuiba;


Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.


Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya duniani, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli?


Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;


Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi katika mkono wa kulia wa Mungu.


Basi, viueni viungo vyenu vilivyo vya kidunia, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;