Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wakolosai 2:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wakolosai 2:3
21 Marejeleo ya Msalaba  

Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.


Kwa kuwa imefichwa mbali na macho ya wote walio hai, Na kusitirika na ndege wa angani.


Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;


Na Roho ya BWANA itakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;


Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonesha njia ya fahamu?


Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.


Na kwa sababu hiyo hekima ya Mungu ilisema, Tazama, nitatuma kwao manabii na mitume, nao watawaua baadhi yao na kuwafukuza,


Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!


bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wagiriki, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.


Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;


Naye alituzidishia hiyo katika hekima yote na ujuzi;


Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;


ambaye sisi tunamhubiri habari zake tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, tupate kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo.


Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;


Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.


Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.


Naam, na kwa sababu iyo hiyo jitahidini sana ili katika imani yenu mtie na wema, na katika wema wenu maarifa,


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.