Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wagalatia 3:24 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, hiyo sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani tufanywe waadilifu mbele yake Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, hiyo sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani tufanywe waadilifu mbele yake Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, hiyo sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani tufanywe waadilifu mbele yake Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hivyo, Torati ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Al-Masihi, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Al-Masihi, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wagalatia 3:24
16 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.


Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani;


Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu elfu kumi katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili.


Lakini tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.


Maana mimi kwa njia ya sheria niliifia sheria ili nimwishie Mungu.


Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi.


mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.