Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wagalatia 2:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wa Mataifa wenye dhambi,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine wenye dhambi!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine wenye dhambi!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine wenye dhambi!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wa Mataifa wenye dhambi,

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wagalatia 2:15
14 Marejeleo ya Msalaba  

Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?


akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kutiwa mikononi mwa wenye dhambi, na kusulubiwa, na kufufuka siku ya tatu.


Naye akaniambia, Nenda zako; kwa kuwa mimi nitakutuma uende mbali kwa watu wa Mataifa.


Ni nini basi? Tu bora kuliko wengine? La! Hata kidogo. Kwa maana tumekwisha kuwashitaki Wayahudi na Wagiriki ya kwamba pia wamekuwa chini ya dhambi;


Kwa hiyo ilitoka katika imani, iwe kwa njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazawa wote; si kwa wale wa torati tu, ila na kwa wale wa imani ya Abrahamu; aliye baba yetu sisi sote;


Lakini ikiwa sisi wenyewe, kwa kutafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, tulionekana kuwa wenye dhambi, je! Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!


ambao zamani, sisi sote nasi tulienda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira, kama wengineo wote.


Lakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu yeyote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi.


Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.


Kisha BWANA akakutuma safarini, akasema, Nenda ukawaangamize kabisa wale Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hadi watakapoangamia.