Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waefeso 6:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waefeso 6:16
16 Marejeleo ya Msalaba  

Baada ya mambo hayo neno la BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako itakuwa kubwa sana.


Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.


Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu.


Naye amemtengenezea silaha za kuua, Akifanya mishale yake kuwa mipini ya moto.


Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.


Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.


Si kwamba tunatawala imani yenu; bali tu wasaidizi wa furaha yenu; maana kwa imani yenu mnasimama.


Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.