Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waefeso 4:26 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Muwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Muwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waefeso 4:26
22 Marejeleo ya Msalaba  

Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.


Muwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.


Tena hao watumishi wako wote wataniteremkia kwangu mimi, nao watanisujudia, wakisema, Toka wewe, na hawa watu wote wakufuatao; na baada ya hayo nitatoka. Basi akatoka kwa Farao na hasira kuu.


Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.


Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.


Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.


Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.


Haruni atakusanywa awe pamoja na watu wake; kwa kuwa hataingia katika nchi niliyowapa wana wa Israeli, kwa sababu mliasi kinyume cha neno langu hapo penye maji ya Meriba.


Bali mimi nawaambieni, Kila amkasirikiaye ndugu yake itampasa hukumu; na mtu akimtusi ndugu yake, anastahili kuhukumiwa na baraza; na mtu akimwambia nduguye, Ewe mpumbavu, anastahili kuingia katika moto wa Jehanamu.


Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.


Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.


mpe ujira wake kwa siku yake, wala jua lisichwe juu yake; kwa maana ni maskini, moyo wake umeutumainia huo; asije akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako.


Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;


kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.


Basi Yonathani akaondoka pale mezani, akiwa na hasira kali, wala hakula chakula siku ya pili ya mwezi, kwa sababu alimhuzunikia Daudi sana, na kwa sababu baba yake amemwaibisha.