Kwa sababu wameniacha mimi, nao wamepafanya mahali hapa kuwa mahali pageni, nao hapa wamewafukizia uvumba miungu mingine wasiowajua, wala wao, wala baba zao, wala wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia;
Waamuzi 5:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Walichagua miungu mipya, Ndipo kulikuwa na vita malangoni; Je! Ilionekana ngao au mkuki Katika watu elfu arubaini wa Israeli? Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Walijichagulia miungu mipya, kukawa na vita katika nchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu 40,000 wa Israeli. Biblia Habari Njema - BHND Walijichagulia miungu mipya, kukawa na vita katika nchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu 40,000 wa Israeli. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Walijichagulia miungu mipya, kukawa na vita katika nchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu 40,000 wa Israeli. Neno: Bibilia Takatifu Mungu alichagua viongozi wapya vita vilipokuja malangoni ya mji; lakini hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa watu elfu arobaini katika Israeli. Neno: Maandiko Matakatifu Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli. BIBLIA KISWAHILI Walichagua miungu mipya, Ndipo kulikuwa na vita malangoni; Je! Ilionekana ngao au mkuki Katika watu elfu arobaini wa Israeli? |
Kwa sababu wameniacha mimi, nao wamepafanya mahali hapa kuwa mahali pageni, nao hapa wamewafukizia uvumba miungu mingine wasiowajua, wala wao, wala baba zao, wala wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia;
Wakamwacha BWANA, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha BWANA, akaghadhibika.
Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za BWANA bali wao hawakufanya hivyo.
Wana wa Israeli wakamlilia BWANA; kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa ya vita; naye akawakandamiza sana wana wa Israeli muda wa miaka ishirini.
Mbali na kelele za hao wapigao mishale, katika mahali pa kuteka maji, Hapo watatangaza matendo ya haki ya BWANA; Naam, matendo ya haki ya kutawala kwake katika Israeli. Ndipo watu wa BWANA waliposhuka malangoni.
Watawala walikoma katika Israeli, walikoma, Hadi mimi Debora nilipoinuka, Nilipoinuka mimi, mama katika Israeli.