Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waamuzi 14:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Samsoni akawaambia, Mimi nitawategea ninyi kitendawili; kama mnaweza kunitegulia katika hizo siku saba za karamu, na kukitambua, ndipo nitakapowapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Samsoni akawaambia, “Nitatega kitendawili. Kama mkiweza kutegua kitendawili hicho kwa muda wa siku saba za sherehe za harusi, basi, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Samsoni akawaambia, “Nitatega kitendawili. Kama mkiweza kutegua kitendawili hicho kwa muda wa siku saba za sherehe za harusi, basi, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Samsoni akawaambia, “Nitatega kitendawili. Kama mkiweza kutegua kitendawili hicho kwa muda wa siku saba za sherehe za harusi, basi, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Samsoni akawaambia, Mimi nitawategea ninyi kitendawili; kama mnaweza kunitegulia katika hizo siku saba za karamu, na kukitambua, ndipo nitakapowapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waamuzi 14:12
22 Marejeleo ya Msalaba  

Akawapa kila mtu nguo za kubadili; lakini Benyamini, alimpa fedha mia tatu na mavazi matano ya kubadili.


Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la BWANA, alikuja ili amjaribu kwa maswali ya fumbo.


Akasema, Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta ya fedha, na mavazi mawili.


Mfalme wa Shamu akasema, Haya! Basi, mimi nitampelekea mfalme wa Israeli waraka. Basi akaenda zake, akachukua mikononi mwake talanta kumi za fedha, na vipande vya dhahabu elfu sita, na mavazi kumi.


Basi, wakati ule Sulemani akafanya sikukuu, na Israeli wote pamoja naye, kusanyiko kubwa sana, toka maingilio ya Hamathi mpaka kijito cha Misri, muda wa siku saba.


Nitatega sikio langu nisikie mithali, Na kufumbua fumbo langu kwa kinubi.


Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao.


Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.


Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli mithali;


Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, wao hunisema; Je! Mtu huyu si mtu mwenye kupiga mithali?


Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.


Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno;


Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.


Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wezi huvunja na kuiba;


Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema,


Basi wanafunzi wake wakasema, Tazama, sasa wasema waziwazi, wala huneni mithali yoyote.


Maana sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.


Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.


Basi ikawa hapo watu walipomwona, wakamletea wenziwe thelathini, wawe pamoja naye.


lakini msipoweza kunitegulia ndipo mtakaponipa mimi mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu. Basi wakamwambia, Haya, tega kitendawili chako, ili tupate kukisikia.