Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 49:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wapiga mishale walimtenda machungu, Wakamlenga na kumbana sana

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Wapiga mishale walimshambulia vikali, wakamtupia mishale na kumsumbua sana.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Wapiga mishale walimshambulia vikali, wakamtupia mishale na kumsumbua sana.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wapiga mishale walimshambulia vikali, wakamtupia mishale na kumsumbua sana.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wapiga mishale walimtenda machungu, Wakamlenga na kumbana sana

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 49:23
12 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamwona akiwa mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue.


wakamtwaa wakamtupa katika shimo; na hilo shimo ilikuwa tupu, hamna maji.


Wakapita wafanya biashara Wamidiani; basi wakamtoa Yusufu, wakampandisha kumtoa katika shimo, wakamuuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande vya fedha ishirini; nao wakamchukua Yusufu mpaka Misri.


Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani.


Wakaambiana, Kweli sisi tulimkosea ndugu yetu, kwa kuwa tuliona shida ya roho yake, alipotusihi, wala hatukusikia, kwa hiyo shida hii imetupata.


Yusufu ni mti mchanga wenye kuzaa, Mti mchanga wenye kuzaa karibu na chemchemi, Matawi yake yametanda ukutani.


Lakini upinde wake ukakaa imara, Mikono yake ikapata nguvu, Kwa mikono ya Mwenye Enzi wa Yakobo; Kwa jina la mchungaji, yeye mwamba wa Israeli,


Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini BWANA akanisaidia.


Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wanaoyalenga maneno ya uchungu kama mishale,


Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.


wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwahimiza wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.