Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 49:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Ee Mwenyezi-Mungu, nangojea uniokoe!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Ee Mwenyezi-Mungu, nangojea uniokoe!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Ee Mwenyezi-Mungu, nangojea uniokoe!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Ee Mwenyezi Mungu, nautafuta wokovu wako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Ee bwana, nautafuta wokovu wako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 49:18
32 Marejeleo ya Msalaba  

Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katika njia, Aumaye visigino vya farasi, Na apandaye akaanguka chali.


Ee BWANA, nimeungojea wokovu wako, Na maagizo yako nimeyatenda.


Ee BWANA, nimeutamani wokovu wako, Na sheria yako ndiyo furaha yangu.


Ee BWANA, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako kulingana na ahadi yako.


Kama vile macho ya watumishi Yanavyoutegemea mkono wa bwana zao Kama macho ya mjakazi Yanavyoutegemea mkono wa bimkubwa wake; Ndivyo macho yetu yanavyomtegemea BWANA, Mungu wetu, Hadi atakapoturehemu.


Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja, Na neno lake nimelitumainia.


Laiti wokovu wa Israeli ungetoka katika Sayuni! BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake; Yakobo atashangilia, Israeli atafurahi.


Nilimngoja BWANA kwa subira, Akaniinamia na kusikia kilio changu.


Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa utulivu, Wokovu wangu hutoka kwake.


Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa utulivu. Maana tumaini langu hutoka kwake.


Ee BWANA, utuoneshe rehema zako, Utupe wokovu wako.


BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.


Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake; Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.


Katika siku hiyo watasema, Tazama, huyu ndiye Mungu wetu, Ndiye tuliyemngoja atusaidie; Huyu ndiye BWANA tuliyemngoja, Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake.


Kwa ajili ya hayo BWANA atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu; kwa maana BWANA ni Mungu wa hukumu; heri wote wamngojao.


Ee BWANA, uturehemu; tumekungoja wewe; uwe wewe mkono wetu kila asububi, na wokovu wetu pia wakati wa taabu.


Basi sasa, tafadhali mpe bwana wangu, mfalme wa Ashuru, dhamana, nami nitakupa farasi elfu mbili, ikiwa wewe kwa upande wako waweza kupandisha watu juu yao.


Nami nitamngojea BWANA, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia.


BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.


Ni mfanya biashara, aliye na mizani ya udanganyifu mkononi mwake; anapenda kudhulumu.


Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.


Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.


akaenda Yusufu, mtu wa Arimathaya, mstahiki, mtu wa baraza ya mashauri, naye mwenyewe anautazamia ufalme wa Mungu; akafanya ujasiri, akaingia mbele ya Pilato akauomba mwili wake Yesu.


Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.


Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.


Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,


(wala hakulikubali shauri na tendo lao), naye ni mtu wa Arimathaya, mji mmoja wa Wayahudi, tena anautazamia ufalme wa Mungu;


Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.


Bali tukikitumainia kitu tusichokiona, twakingojea kwa subira.


Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.


na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu, mwenye kutuokoa kutoka kwa ghadhabu itakayokuja.