Lea akasema, Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu. Akamwita jina lake Isakari.
Mwanzo 49:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Isakari ni punda hodari, Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo; Matoleo zaidiBiblia Habari Njema “Isakari ni kama punda mwenye nguvu, ajilazaye kati ya mizigo yake. Biblia Habari Njema - BHND “Isakari ni kama punda mwenye nguvu, ajilazaye kati ya mizigo yake. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza “Isakari ni kama punda mwenye nguvu, ajilazaye kati ya mizigo yake. Neno: Bibilia Takatifu “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake. Neno: Maandiko Matakatifu “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake. BIBLIA KISWAHILI Isakari ni punda hodari, Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo; |
Lea akasema, Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu. Akamwita jina lake Isakari.
Akaona mahali pa raha, kuwa pema, Na nchi, ya kuwa ni nzuri, Akainama bega lake lichukue mizigo, Akawa mtumishi kwa kazi ngumu.
Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, Mbawa zake ziking'aa kama fedha Na manyoya yake kama dhahabu?
Basi wakamwendea karibu, na kusema, Sisi tutafanya mazizi hapa kwa ajili ya mifugo yetu, na kujenga miji kwa ajili ya watoto wetu;
Na Zabuloni akamnena, Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako; Na Isakari, katika hema zako.
Baada yake Abimeleki, akainuka Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, kuwaokoa Israeli; naye alikuwa akikaa Shamiri, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu.