Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 39:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala kuwa naye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Huyo mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, lakini Yosefu hakumsikiliza wala kukubali kulala naye kamwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Huyo mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, lakini Yosefu hakumsikiliza wala kukubali kulala naye kamwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Huyo mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, lakini Yosefu hakumsikiliza wala kukubali kulala naye kamwe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yusufu siku baada ya siku, Yusufu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yusufu siku baada ya siku, Yusufu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala kuwa naye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 39:10
21 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani afanye kazi yake, na hapakuwa na mtu yeyote kati ya wale wa nyumbani karibu;


Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.


Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu chochote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nimkosee Mungu?


Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.


Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;


Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na BWANA atatumbukia ndani yake.


Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni mtego wa shimo jembamba.


Naam, huotea kama mnyang'anyi; Huwaongeza wenye hila katika wanadamu.


Maana midomo ya malaya hudondosha asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta;


Itenge njia yako mbali naye, Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.


Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya,


Wapate kukulinda na malaya, Na mwasherati akubembelezaye kwa maneno yake.


Hukaa mlangoni pa nyumba yake, Juu ya kiti mahali pa mjini palipoinuka,


Kila aliye mjinga na aingie humu. Tena amwambia mtu aliyepungukiwa na akili,


Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.


Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.


jitengeni na ubaya wa kila namna.


Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, watunze nyumba zao; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.


Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.


Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.