Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mhubiri 7:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini pia, usiwe mwovu sana wala usiwe mpumbavu! Ya nini kufa kabla ya wakati wako?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini pia, usiwe mwovu sana wala usiwe mpumbavu! Ya nini kufa kabla ya wakati wako?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini pia, usiwe mwovu sana wala usiwe mpumbavu! Ya nini kufa kabla ya wakati wako?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mhubiri 7:17
15 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Daudi akarudi ili awabariki watu wa nyumbani mwake. Na Mikali, binti Sauli, akatoka nje aende kumlaki Daudi, naye akasema, Mfalme wa Israeli alikuwa mtukufu leo namna gani, akijifunua mwili wake mbele ya vijakazi vya watumishi wake, mfano wa watu baradhuli mmojawapo, ajifunuavyo mwili wake mbele ya watu, asipokuwa na haya!


Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao, Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji;


Nawe, Ee Mungu, utawateremsha, Wafikie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.


Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.


Pamoja na hayo uliwatwaa wana wako na binti zako, ulionizalia, ukawatoa sadaka kwao ili waliwe. Je! Mambo yako ya kikahaba ni kitu kidogo tu,


Basi, akaniambia, Umeyaona haya, Ee mwanadamu? Je! Ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda, wayafanye machukizo wanayoyafanya hapa? Kwa maana wameijaza nchi hii udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na, tazama, wanaliweka tawi puani.


Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na wadudu, akatokwa na roho.


Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tuko hapa.


Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.


Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.


Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu.


Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, BWANA alimpiga huyo Nabali, hadi akafa.