Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuulizauliza habari.
Mhubiri 5:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Ni afadhali kutoweka nadhiri kuliko kuweka nadhiri kisha usiitimize. Biblia Habari Njema - BHND Ni afadhali kutoweka nadhiri kuliko kuweka nadhiri kisha usiitimize. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Ni afadhali kutoweka nadhiri kuliko kuweka nadhiri kisha usiitimize. Neno: Bibilia Takatifu Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize. Neno: Maandiko Matakatifu Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize. BIBLIA KISWAHILI Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe. |
Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuulizauliza habari.
au, kama mtu akijiapisha, kwa kutamka haraka kwa midomo yake, kutenda uovu, au kutenda mema, neno lolote mtu atakalolitamka kwa kiapo pasipo kufikiri, bila kujua; hapo atakapolijua, ndipo atakapokuwa na hatia katika mambo hayo mojawapo;
Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA.
Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa BWANA wa majeshi.
Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.
Utakapoweka nadhiri kwa BWANA, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.
Ikawa alipomuona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia BWANA kinywa changu, nami siwezi kurudi nyuma.