Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mhubiri 12:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Umkumbuke kabla ya wakati ambapo kwako mwanga wa jua utafifia; mwezi na nyota haviangazi tena, nayo mawingu yametanda tena baada ya mvua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Umkumbuke kabla ya wakati ambapo kwako mwanga wa jua utafifia; mwezi na nyota haviangazi tena, nayo mawingu yametanda tena baada ya mvua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Umkumbuke kabla ya wakati ambapo kwako mwanga wa jua utafifia; mwezi na nyota haviangazi tena, nayo mawingu yametanda tena baada ya mvua.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mhubiri 12:2
15 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa.


Na macho ya Israeli yalikuwa mazito kwa uzee, wala hakuweza kuona vizuri. Akawaleta kwake, naye akawabusu, na kuwakumbatia.


Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maporomoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.


Wewe, uliyetuonesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Kutoka katika vina virefu chini ya nchi.


Ee Mungu, yale maji yalikuona, Yale maji yalikuona, yakaogopa. Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,


Miaka ya maisha yetu ni sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Tena kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana wakati unapita upesi nasi kutokomea punde.


Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.


Nao watanguruma juu yao siku hiyo Kama ngurumo ya bahari; Na mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki Nayo nuru imetiwa giza katika mawingu yake.


Jua na mwezi vimetiwa giza, na nyota zimeacha kuangaza.


Lakini mara tu, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;


Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),


Basi Eli umri wake umepata miaka tisini na minane; na macho yake yamepofuka hata asiweze kuona.


Ikawa alipolitaja sanduku la Mungu, Eli akaanguka kitini pake kwa nyuma, kando ya mlango, shingo yake ikavunjika, akafa; maana alikuwa mzee, tena mzito. Naye alikuwa amewaamua Waisraeli miaka arubaini.