Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 8:36 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Asiyenipata anajidhuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Asiyenipata anajidhuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Asiyenipata anajidhuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanaonichukia mimi hupenda mauti.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 8:36
20 Marejeleo ya Msalaba  

Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Ikiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?


Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.


Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.


Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.


Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.


Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.


Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.


Kuonekana kwa nyuso zao kwashuhudia juu yao, wafunua dhambi yao kama Sodoma, hawaifichi. Ole wa nafsi zao, kwa maana wamejilipa nafsi zao uovu.


Mbona mnataka kufa, wewe na watu wako, kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni, kama BWANA alivyosema katika habari ya taifa lile, lisilotaka kumtumikia mfalme wa Babeli?


Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa; jifanyieni moyo mpya na roho mpya; mbona mnataka kufa, enyi nyumba ya Israeli?


Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?


Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona ninyi wenyewe kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.


Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tuko hapa.


Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maranatha.


Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?


sisi je! Tutapataje kupona, tukipuuza wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliomsikia;