Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 31:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mume wake ni mtu mashuhuri barazani, anakoshiriki vikao vya wazee wa nchi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mume wake ni mtu mashuhuri barazani, anakoshiriki vikao vya wazee wa nchi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mume wake ni mtu mashuhuri barazani, anakoshiriki vikao vya wazee wa nchi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 31:23
8 Marejeleo ya Msalaba  

Wakati nilipotoka kwenda mjini, kupitia langoni, Nilipokitengeza kiti changu katika njia kuu,


Mwanamke mwema ni taji la mumewe; Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.


Kwa mpumbavu hekima haipatikani; Hafumbui kinywa chake langoni.


Weka waamuzi na maofisa katika malango yako yote akupayo BWANA, Mungu wako, kwa hesabu ya kabila zako; nao wawaamue watu kwa maamuzi ya haki.


ndipo babaye na mamaye na wamkamate, na kumpeleka kwa wazee wa mji wake, katika lango la mahali pake;


Basi Boazi akakwea kwenda mpaka langoni, akaketi pale; na tazama, yule mtu wa jamaa aliyekuwa karibu, ambaye Boazi amemnena, akapita. Naye akamwita, Haya! Wewe, karibu, uketi hapa. Naye akaja akaketi.


Na watu wote waliokuwapo langoni, na wale wazee, wakasema, Naam, sisi ni mashahidi. BWANA na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wawili walioijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrata, na kuwa mashuhuri katika Bethlehemu.


Kisha akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, Ninyi nanyi, ketini hapa. Wakaketi.