Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 30:30 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hatishwi na mwingine yeyote yule;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

simba: Mnyama mwenye nguvu kuliko wote, wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

simba: Mnyama mwenye nguvu kuliko wote, wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

simba: mnyama mwenye nguvu kuliko wote, wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

simba, mwenye nguvu miongoni mwa wanyama, wala haogopi chochote;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

simba, mwenye nguvu miongoni mwa wanyama, asiyerudi nyuma kwa chochote;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hatishwi na mwingine yeyote yule;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 30:30
7 Marejeleo ya Msalaba  

Sauli na Yonathani walipendwa na kupendeza Maishani wala mautini hawakutengwa; Walikuwa wepesi kuliko tai, Walikuwa hodari kuliko simba.


Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.


Jogoo anayetamba; na beberu; Na mfalme asimamaye mbele ya watu wake.


Mwanadamu, mfanyie Farao, mfalme wa Misri, maombolezo, umwambie, Ulifananishwa na mwanasimba wa mataifa; lakini umekuwa kama joka katika bahari; nawe watoka kwa nguvu pamoja na mito yako, na kuyachafua maji kwa miguu yako, na kuitia uchafu mito yao.


Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya mataifa, kati ya kabila nyingi, mfano wa simba kati ya wanyama wa msituni, kama mwanasimba kati ya makundi ya kondoo, ambaye, akiwa anapita katikati, hukanyagakanyaga na kuraruararua, wala hakuna wa kuokoa.


Tazama, watu hawa wanaondoka kama simba jike, Na kama simba anajiinua nafsi yake, Hatalala hadi atakapokula mawindo, Na kunywa damu yao waliouawa.


Nao watu wa mji wakamwambia siku ya saba kabla ya jua kuchwa, Ni kitu gani kilicho tamu kuliko asali? Ni kitu gani kilicho na nguvu kuliko simba? Naye akawaambia, Msingelima na mtamba wangu, Hamngekitegua kitendawili changu.