Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 30:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kama mtu akimdhihaki baba yake, na kudharau utii kwa mama yake, kunguru wa bondeni watamdonoa macho, na kuliwa na tai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kama mtu akimdhihaki baba yake, na kudharau utii kwa mama yake, kunguru wa bondeni watamdonoa macho, na kuliwa na tai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kama mtu akimdhihaki baba yake, na kudharau utii kwa mama yake, kunguru wa bondeni watamdonoa macho, na kuliwa na tai.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Jicho lile limdhihakilo baba, lile linalodharau kumtii mama, litang’olewa na kunguru wa bondeni, litaliwa na tai.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Jicho lile limdhihakilo baba, lile linalodharau kumtii mama, litang’olewa na kunguru wa bondeni, litaliwa na tai.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 30:17
14 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Rispa, binti Aya, akatwaa nguo ya magunia akajitandikia mwambani, tangu mwanzo wa mavuno hadi waliponyeshewa mvua toka mbinguni; wala hakuacha ndege wa angani kukaa juu yao mchana, wala wanyama wa mwitu usiku.


Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye.


Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.


Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.


Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao.


Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.


Kwa maana kila mtu amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa, amemlaani baba yake na mama yake; damu yake itakuwa juu yake.


Mwana humheshimu baba yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? BWANA wa majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau jina lako kwa jinsi gani?


Na mzoga wako utakuwa chakula cha ndege wote wa angani, na wanyama wote wa duniani, pasiwe na mtu wa kuwafukuza.


Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.