Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenye kumbembeleza jirani yake, anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenye kumbembeleza jirani yake, anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenye kumbembeleza jirani yake, anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:5
18 Marejeleo ya Msalaba  

Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo, Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi.


Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;


Kwa maana hujipendekeza machoni pake Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.


Maana vinywani mwao hamna uaminifu; Moyo wao ni shimo tupu, koo lao ni kaburi wazi, Ulimi wao hujipendekeza.


Kwa kuwa mtego hutegwa bure, Mbele ya macho ya ndege yeyote.


Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.


Ulimi unenao uongo huwachukia wale uliowajeruhi; Na kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.


Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.


Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.


Wapate kukulinda na malaya, Na mwasherati akubembelezaye kwa maneno yake.


Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu, Nao umeishinda; Ametandika wavu aninase miguu, Amenirudisha nyuma; Amenifanya kuwa mtu wa pekee, Na mgonjwa mchana kutwa.


Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.


Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe; na kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu.


Maana hatukuwa na maneno ya kujipendekeza wakati wowote, kama mjuavyo, wala maneno ya juu juu ya kuficha choyo; Mungu ni shahidi.


Nao watumishi wa Sauli wakanena maneno hayo masikioni mwa Daudi. Daudi akasema, Je! Ninyi mnaona kuwa ni shani mimi kuwa mkwewe mfalme, nami ni maskini, tena sina cheo?