Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe, lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe, lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe, lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:23
28 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.


Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo.


Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.


Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.


Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini, Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.


Apendaye ugomvi hupenda dhambi; Auinuaye sana mlango wake hutafuta uharibifu.


Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?


Basi, yeyote ajinyenyekezaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.


Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.


Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na wadudu, akatokwa na roho.


aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.