Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waadilifu wakitawala watu hufurahi, lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waadilifu wakitawala watu hufurahi, lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waadilifu wakitawala watu hufurahi, lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:2
16 Marejeleo ya Msalaba  

Matarishi wakaondoka wakaenda haraka kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. Mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa divai; bali mji wa Shushani ukafadhaika.


Naye Mordekai akatoka usoni pa mfalme, amevaa mavazi ya kifalme, ya rangi ya samawati na nyeupe, mwenye taji kubwa la dhahabu, na joho la kitani safi na rangi ya zambarau. Mji wa Susa wakapaza sauti, wakashangilia.


Ili huyo mpotovu asitawale, Wala pasiwe na wa kuwatega watu.


Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi; Waovu wanapoangamia, watu hushangilia.


Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi; Bali waovu waondokapo, watu hujificha.


Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.


Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.


Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye;


ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.


Kisha nikarudi na kuona udhalimu wote unaotendeka chini ya jua; na tazama, machozi yao waliodhulumiwa, ambao walikuwa hawana mfariji; na upande wa wale waliowadhulumu kulikuwa na uwezo, lakini wale walikuwa hawana mfariji.


Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale majusi, alighadhibika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wa kiume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake kote, kuanzia wenye miaka miwili na chini yake, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale majusi.


Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.


Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.